Mamia ya Wayahudi wanaofuata
dini yao kiasilia, wamepambana na polisi karibu na Jerusalem kwa sababu
ya mvutano kuhusu kuwatenga wanawake na wanaume.
Afisa mmoja wa polisi alijeruhiwa katika mji wa
Beit Shamesh, wakati polisi walipoitwa kuondoa ilani kwenye barabara
kuu, inayoamrisha wanawake wajitenge na wanaume. Makundi ya Wayahudi wanaofuata dini yao kiasili waliwafukuza polisi na kuwarushia mawe. Ghasia hizo ndio za karibuni kabisa katika
mfululizo wa matukio mengine nchini Israil, ambapo wanawake
walilazimishwa kukaa nyuma kwenye mabasi, katika maeneo ya Wayahudi hao,
ingawa mahakama yametoa amri kuwa wanaweza kukaa watakapo.
0 Comments