10,000 waliofaulu Morogoro wakosa nafasi sekondari

WATAHINIWA 9,726 sawa na asilimia 32 waliofanya mtihani wa kuhitimu masomo ya darasa la saba mwaka huu na kufaulu , wamekosa nafasi ya kuendelea na masomo ya Kidato cha kwanza mwakani kutokana na uhaba wa vyumba 245 vya madarasa kwenye shule za sekondari mkoani Morogoro.

Ofisa Elimu wa Mkoa wa Morogoro, Fatma Kilimia, alitoa taarifa juzi wakati wa kikao cha uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza mwakani.


Kilimia alisema kuwa kati ya waliokosa nafasi za kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza licha ya kufaulu mitihani yao.


“ Tujipange kuwezesha kujenga madarasa haya ,tusisahau pia suala la vyoo na nyumba za walimu na ujenzi huu uwe umekamilika kabla ya Februari mwakani, ili watoto wasichelewe katika masomo yao,” alisema Kilimia.


Alisema wanafunzi walioandikishwa Machi mwaka huu kwa ajili ya kufanya mtihani walikuwa ni 51,775 kati ya hao wavulana 24,979 na wasichana walikuwa ni 26,796.


Wanafunzi 869 kati yao wavulana 468 na wasichana 401 walishindwa kufanya mitihani kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vifo, utoro na mimba.


Kwa mujibu wa Ofisa Elimu wa Mkoa huo, wanafunzi waliochaguliwa ni 30,808. Wavulana ni 15,161 na wasichana 15,647.


Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Halima Dendego, aliwataka wakurugenzi watendaji kwa kushirikiana na madiwani pamoja na wananchi kutumia muda mfupi uliobakia kujenga vyumba vya madarasa vinavyohitajika ili kuwezesha watoto wote waliofaulu kuingia darasani kabla ya muhula wa mwaka wa masomo kuanza.

Post a Comment

0 Comments