HABARI ZA KIMATAIFA


 

Mjumbe maalum wa Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (SRCC) nchini Somalia, Balozi Mahamat Saleh Annadif ameshutumu vikali shambulio la kigaidi lililofanywa leo na magaidi wa Al-Shabaab katika makao ya Umoja wa Mataifa mjini Mogadishu.
"Tunalaani vikali shambulio hili la kinyama katika makao ya Umoja wa Mataifa mjini Mogadishu. Mashambulio haya yasiyofanikiwa yanayoendeshwa na Al-Shabaab yanalenga tu kuvuruga jitihada zinazochukuliwa na wananchi wa Somalia baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa zaidi ya ishirini na magaidi hao hawawezi kuzuia jitihada zetu za pamoja kuendelea kuwasaidia wananchi wa Somalia kuijenga nchi yao" amesema Mwakilishi Maalum wa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika nchini Somalia (SRCC), Balozi Mahamat Saleh Annadif. 
kwa  habari  zaidi  BONYEZA HAPA

Post a Comment

0 Comments