HABARI ZA KIMATAIFA

Mjumbe maalum wa Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa 
Afrika (SRCC) nchini Somalia, Balozi Mahamat Saleh Annadif ameshutumu 
vikali shambulio la kigaidi lililofanywa leo na magaidi wa Al-Shabaab 
katika makao ya Umoja wa Mataifa mjini Mogadishu.
                     "Tunalaani vikali shambulio hili la kinyama 
katika makao ya Umoja wa Mataifa mjini Mogadishu. Mashambulio haya 
yasiyofanikiwa yanayoendeshwa na Al-Shabaab yanalenga tu kuvuruga 
jitihada zinazochukuliwa na wananchi wa Somalia baada ya vita vya 
wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa zaidi ya ishirini na magaidi hao 
hawawezi kuzuia jitihada zetu za pamoja kuendelea kuwasaidia wananchi wa
 Somalia kuijenga nchi yao" amesema Mwakilishi Maalum wa Mwenyekiti wa 
Umoja wa Afrika nchini Somalia (SRCC), Balozi Mahamat Saleh Annadif. kwa habari zaidi BONYEZA HAPA


0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home