JAMANI WATAALAM WA KUJINYONGA MPO? SOMA HABARI HII YA KUTISHA. KISHA TOA MAONI NA MTAZAMO WAKO.


Mchungaji wa kanisa moja huko California Marekani, Harold Camping, ametabiri kuwa Mei 21,2011 saa moja kamili usiku mwisho wa dunia, na huenda tusiione tena jumapili ya wiki ijayo, kwani dunia itakuwa imefika mwisho  wake siku hiyo ya Jumamosi.

Mchungaji Camping kwa kutumia mahesabu ya tarehe na mafunzo ya Biblia, ametabiri kuwa kiama kitakuwa jumamosi, na miezi mitano baadae kwenye tarehe 21 Oktoba, Mungu ataiteketeza dunia.

 Mchungaji Camping ambaye anamiliki radio ya Christian Family Network yenye mtandao mkubwa sana nchini humo na sehemu zingine duniani ikiwa inarusha matangazo kwa lugha zaidi 48 zikiwemo lugha kutoka Afrika Kusini.
Camping mwenye umri wa miaka 89 ana wafuasi wengi sana duniani na sasa anaendesha kampeni kubwa kuwajulisha watu kuhusu mwisho wa dunia hapo Mei 21.







agari yenye mabango yenye ujumbe mwisho wa dunia Mei 21 yamekuwa yakionekana sehemu mbalimbali za Marekani yakitangaza kuwa mwisho wa dunia ni Mei 21 kwa sababu itakuwa ni siku ya 722 500 tangu Yesu aliposulubiwa msalabani mnamo Aprili moja AD33.
Aidha  Mchungaji Camping amesisitiza kuwa kuwa namba 722 500 ni muhimu sana kwa wakristo duniani kwani inapatikana kwa kuzizidisha namba tatu tukufu (5, 10, 17) mara mbili {5x10x17x5x10x17}

Hii sio mara ya kwanza kwa mchungaji Camping kutabiri matukio makubwa duniani coz Septemba 6 mwaka 1994 akiwa na wafuasi wake wengi walikusanyika mbele ya ukumbi wa Alameda wakisubiri kurudi kwa Yesu Kristo ambaye hakutokea na tangu wakati huo,camping amesema kuwa wamefanya utafiti mkubwa sana na hivyo wana uhakika safari hii utabiri wao utakuwa sahihi.

Kwa habari zaidi bonyeza hapa>>>>> 

Post a Comment

0 Comments