{KIMATAIFA}Mubarak atozwa faini dola milioni 90....

Mahakama ya Misri yameamrisha faini ya dola milioni 90, atozwe rais wa zamani, Hosni Mubarak, pamoja na maafisa wake wawili, kwa kukata huduma za simu za mkononi wakati wa maandamano dhidi ya serikali mwezi wa Januari.
Hosni Mubaraka na mkewe, Heidi, na watoto Gamal (kulia, na Alaa
Hiyo ndiyo hukumu ya mwanzo ya mahakama dhidi ya Bwana Mubarak.
Kiongozi huyo wa zamani anakabili mashtaka makubwa zaidi, kama kuamrisha waandamanaji kuuwawa, ambayo adhabu yake inaweza kuwa kifo.
Maafisa wawili waliotozwa faina na Bwana Mubarak ni waziri mkuu wa zamani, Ahmed Nazif, na waziri wake wa mambo ya ndani ya nchi, Habib al-Adly.



                                                                                                                                                             

 HUKO  LIBYA  TENA

NATO imeshambulia nyumba ya Gaddafi

NATO inasema kuwa imeangamiza minara ya walinzi katika eneo la nyumba ya Kanali Gaddafi wa Libya mjini Tripoli, kwa mashambulio mawili yaliyofanywa na ndege za umoja huo wa kijeshi.
Watu wakizungumza karibu na jumba la Gaddafi la Babu al_aziziya baada ya kushambuliwa mwezi Aprili
Waandishi wa habari mjini Tripoli, wanasema shambulio moja lilofanywa mchana, lilivunja sehemu za ukuta unaozunguka jengo la jeshi la Bab al-Aziziya.
Msemaji wa NATO, alieleza kuwa shambulio hilo ni funzo kubwa kwa kiongozi wa Libya, kwamba hawezi tena kujificha nyuma ya kuta ndefu.

Post a Comment

1 Comments

Anonymous said…
KAZI WANAYO NI KWAMBA GADAFI HANA UJANJA TENA. KAMA VIPI C AACHIE NGAZI TU... ANACHONG'ANG'ANIA NI KITU GANI..