Shirika la Umeme Tanzanian lapata mkopo kuzuia kukatika kwa umeme:











Benki tatu zimekubali kutoa mkopo wa shilingi bilioni 408 (Dola za Marekani 256) kwa Shirika la Umeme Tanzania kwaajili ya mpango wa dharula wa kuzuia kukatika kwa umeme, gazeti la Daily News la Tanzania liliripoti Jumatatu (tarehe 19 Machi).Fedha hizo zitasaidia kununua mafuta mazito kwaajili ya mitambo inayotumia mafuta mazito hayo, alisema William Mhando, mkurugenzi mkuu wa Shirika la Uzalishaji na Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO). "Tunatarajia kupata fedha hizo wili lijalo."
Kampuni inafanya kazi katika "changamoto ya muda" kukarabati miundombinu ya umeme nchi nzima, Mhando alisema, aliongeza kwamba uzalishaji umeshuka hadi megawati 718 kutoka megawati 1200. Alisema shirika la umeme halifanyi mgao wa umeme na tatizo lolote linatokana na mfumo mbaya wa miundombinu. "Hakukuwa na uwekezaji madhubuti katika eneo hili kwa muda mrefu," alisema.
City Bank Tanzania, National Microfinance Bank na National Bank of Commerce zinatoa mkopo kwaajili ya mradi huo.

Post a Comment

1 Comments