(FIKRA MBADALA) NINI KIFANYIKE KUONDOKANA NA MAAFA KAMA HAYA?

Katika  kipindi  kilichopita ndugu  zetu  walipoteza  maisha  kwa  mafuriko  na  hii  yote  ni  kutokana  na  kukosa  maarifa. na  walioathirika  zaidi  na  mafuriko  yale  asilimia  kubwa   ni  wapangaji.  ila  wenye  nyumba  ni  asilimia  ndogo  sana.  kwa  hiyo  napenda  kusema  kuwaondoa  wananchi  katika  maeneo  ya  bondeni  kiukweli  inakua  ngumu  sana   kutokana  kwamba  kunabaadhi  ya  watu  wanakaa  bondeni kwa  kukimbia  gharama  za  kode  za  vyumba.  mfano  mmoja  hivi  majuzi  mwangajamii  imefanya  uchunguzi  na  kugundua  vyumba  vingi  vya  bondeni  bei  zake  ni  ndogo  ukilinganisha  na  visivyo  vya  bondeni  gharama  zake  ni   kubwa.  na  ndio  maana  wananchi  wenye  kipato  cha  chini ndio wanakimbilia  mambondeni. na  endapo  mvua  zikanyesha  wanakuwa  matatizoni.  nataka  kuipatia serikali  ushauri.  kama  kuna uwezekano    maeneo  ya mabondeni serikali  Ichimbe mitaro mikubwa  ambayo  itaelekeza  maji   kwenda baharini pale  mvua  zitakaponyesha.... Tusikubali  watanzania  wafe  kwa  kukosa maarifa  na  ikiwezekana  hata  michango  ipita  kwa  wale  wote  wanaishi  mambondeni  ili  kukamilisha programu  hiyo..

Post a Comment

0 Comments