MTOTO WA AFRIKA MBONA WANATESEKA NA WAKATI AFRIKA NI YAKWAO!!!?

MTOTO  WA  KIAFRIKA  ANAANGAMIA  HUKU  SISI  AMBAPO  TUNANAFASI  TUNAWAANGALIA  NA  KUWATUNGIA  MAJINA  YA AJABU.  TUWASAIDIE  WATOTO  WA AFRIKA NAKUMBUKA WEWE  MAMA,BABA,KAKA DADA,KAMA  MAISHA  YAKO  NI  MAZURI  BASI  MCHUKUE  INGALAU  HATA  MTOTO  YATIMA  MMOJA. NA  MWINGINE  VIVYOHIVYO  YATIMA  WATAONEKANA  WAPI.  JIBU  NI  HAKUNA.. PLEASE  MWAFRIKA  MWENZANGU.. KUMBUKA  YOTE  LAKINI  YATIMA  NDIO IWE  JAMBL  LA  KWANZA.

Nikweli kwamba, maana halisi ya Yatima ni mtoto  aliyefiwa na wazazi.
Nenda ikawa kampotezapoteza mzazi mmoja, bado ataitwa Yatima wa mzazi mmoja.

Bila shaka wote twajua yakuwa Watoto hawa pia wanahaki yakuishi, ambayo haki hiyo inasisitizwa na Mungu baba mwenyewe; Kasema Yeye ni baba wa Yatima.

Watoto hawa, baada yakupoteza wazazi nakukosa msaada; hutafuta namna yakuishi.

Wanaposhindwa, kwakukosa mahali pakuishi nakulala, huondoka nakwenda mitaani kujiifadhi.
JAMBO LAKUSHANGAZA !

Kuliko sisi kuungana pamoja kwa pamoja, tuwasaidie Watoto hawa, tunawapa majina mengine kama
" Watoto wa mitaani "

Swali linakujaJe ? " KUNA MTAA WOWOTE UNAOFAHAMIKA, ULIOBEBA UJAUZITO NAKUZAA MTOTO? "
Jibu ni HAPANA.

hawa Watoto wanahitaji pia upendo wa kweli, nakutambuliwa na Jamii. na wanapokosa hayo, Huwasababishia maumivu moyoni; JAMBO ambalo ,kwakutaka kusahau kwa lazma, huwapeleka kuvuta Gundi, Bangi na Pombe.
Je? HATUWEZI KUWASAIDIA HAWA?
Ndiyo... Tunaweza KUWASAIDIA, kwakutumia kidogo kidogo tulicho nacho nakuwapa wao pia.

Kuwaonyesha upendo wa kweli nakuwafundisha maagizo ya Mungu; pia Kuwaonyesha maadhara ya madawa yakulevya.

Post a Comment

0 Comments