May 28, 2011

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIMKABIDHI ZAWADI YA KINYAGO WAZIRI MKUU WA INDIA.




Image
Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi zawadi ya kinyago Waziri Mkuu wa India, Dk Manmohan Singh wakati Waziri Mkuu huyo alipokutana naye Ikulu, Dar es Salaam. Waziri Mkuu huyo anatarajiwa kurejea nchini kwake Mei 28

May 27, 2011

MAONI YANGU BINAFSI.....

MALUMBANO YA  JANA  YALIYOKUWA  YAKIRUSHWA NA  ITV  KUHUSU  NINI  KIFANYIKE  NINI  ILI KUZUIA  AJALI,   NI   ABIRIA   MWENYE  AWE  ANASHIRIKIANA  NA JESHI  LA POLISI  KATIKA   KUONDOA  ONGEZEKO  LA  AJALI    BARABARANI...       NI  MCHANGO  WANGU    TU  HUO..

May 24, 2011

[KIMATAIFA]>>>>>Na huko sudan wenye silaha Sudan 'wachoma moto Abyei...

Majeshi ya Sudan Kusini

^Wakimbizi wakiukimbia mji wa Abyei^
Majeshi ya kutunza amani ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan yamesema mji unaozozaniwa uliopo mpakani Abyei umechomwa moto tangu ulipotekwa na majeshi kutoka kaskazini.
Umesema majeshi ya Sudan, yanayoitii serikali ya kaskazini, yalikuwa na jukumu la kuhakikisha sheria inafuatwa Abyei.
Takriban wakazi 20,000 wameukimbia mji huo katika siku za hivi karibuni.
Abyei umekuwa na hali ya wasiwasi mkubwa tangu upande wa kusini kupiga kura mapema mwaka huu kutaka kujitenga na upande wa kaskazini.
Baraza la usalama la umoja wa mataifa linatarajiwa kujadili mtafaruku huo na Rais wa Sudan kusini.