December 16, 2011

10,000 waliofaulu Morogoro wakosa nafasi sekondari

WATAHINIWA 9,726 sawa na asilimia 32 waliofanya mtihani wa kuhitimu masomo ya darasa la saba mwaka huu na kufaulu , wamekosa nafasi ya kuendelea na masomo ya Kidato cha kwanza mwakani kutokana na uhaba wa vyumba 245 vya madarasa kwenye shule za sekondari mkoani Morogoro.

Ofisa Elimu wa Mkoa wa Morogoro, Fatma Kilimia, alitoa taarifa juzi wakati wa kikao cha uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza mwakani.


Kilimia alisema kuwa kati ya waliokosa nafasi za kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza licha ya kufaulu mitihani yao.


“ Tujipange kuwezesha kujenga madarasa haya ,tusisahau pia suala la vyoo na nyumba za walimu na ujenzi huu uwe umekamilika kabla ya Februari mwakani, ili watoto wasichelewe katika masomo yao,” alisema Kilimia.


Alisema wanafunzi walioandikishwa Machi mwaka huu kwa ajili ya kufanya mtihani walikuwa ni 51,775 kati ya hao wavulana 24,979 na wasichana walikuwa ni 26,796.


Wanafunzi 869 kati yao wavulana 468 na wasichana 401 walishindwa kufanya mitihani kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vifo, utoro na mimba.


Kwa mujibu wa Ofisa Elimu wa Mkoa huo, wanafunzi waliochaguliwa ni 30,808. Wavulana ni 15,161 na wasichana 15,647.


Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Halima Dendego, aliwataka wakurugenzi watendaji kwa kushirikiana na madiwani pamoja na wananchi kutumia muda mfupi uliobakia kujenga vyumba vya madarasa vinavyohitajika ili kuwezesha watoto wote waliofaulu kuingia darasani kabla ya muhula wa mwaka wa masomo kuanza.

MALI YA TAIFA.. ISIYOKUWA NA FAIDA KWA MWANANCHI.

TWIGA

December 15, 2011

UBOVU WA BARABARA MAENEO YA SINZA.

Maeneo ya sinza.
 Kiukwe  naweza  kusema  hii  imekuwa  kero  kubwa  sana  maeneo  ya  sinza kuanzia  hapa  kijueni  kurudi  nyuma  kamaunarudi  pande  za  magomeni  kiukweli  barabara  ni  mbovu !! mbovu!!   mbovu!!! kupita  kiasi. hii   ni  kasumba  kubwa  sana.  na  ukiuliza. kwanini  barabara  wakazi  wa  maeneo  hayo.  wanakwambia  wamechoshwa  na  ahadi  za  viongozi  wao.    kitaswira  na  kimuonekano ni  kwamba   viongozi  wetu  pale  wanapotaka  kura  zenu. utumia  neno  la  kusema hivi. barabara  juu  na chini. ili  tu  wananchi  waamini.  lakini  sasa imekuwa  kero  sana  hasa  kwa  wakazi  wa   sinza. na ukiuliza  je  viongozi  hao  huwa  wanapita   maeneo  hayo.  wakazi  hao  watakujibu  ndio.  lakini  hii  inatokana  na  dharau  za  viongozi  wetu  kwa  kuwadharau    wananchi. viongozi  hao  wamekuwa  wakipita  na  magari  yao  ya  kifahari  yaliyo tokana  pesa  za  wananchi.  nakumbuka    kipindi  cha  kampeni kuna kiongozi  alitamka  neno  hili.    nitajenga  barabra  zote  kwa  kiwango  cha  lami.  na  pia  barabara  za  juu.     Lakini sasa  imekuwa kwamba  kama  kiongozi  atatoa   ahadi  za  uongo.  na asitekeleze  je  wananchi  watamuamini  tena?  jibu  ni  hapana.  kiukweli   kama  mtu  au  kiongozi  hawezi  kutekeleza jambo  ni  bora  asema  hivi,  nitatoa  huduma  kwa  kadiri  nitakavyo  weza. aliye yasema  maneno  hayo  ni  rais  wetu.  siwezi  kuacha  kumtaja  maana  nisipo mtaja  nitakuwa  mnafiki...  Jamani  viongozi  inaonyesha  hata  familiya  zenu  mnazidanganya  hivyo.  kama  uongo  na ahadi kama  hivi  mtaendelea  nazo.  kiukweli mnapeleka  taifa kubaya  sana  na  si  kingine  ni  kizai  kijacho.  HII  NI  CHANGA  MOTO  KWA  VIONGOZI.  NAWAOMBA  HIZO  PAMBA  MLIZO  WEKA  MASIKIONI  ZITOENI.