10,000 waliofaulu Morogoro wakosa nafasi sekondari
WATAHINIWA 9,726 sawa na asilimia 32 waliofanya mtihani wa kuhitimu
masomo ya darasa la saba mwaka huu na kufaulu , wamekosa nafasi ya
kuendelea na masomo ya Kidato cha kwanza mwakani kutokana na uhaba wa
vyumba 245 vya madarasa kwenye shule za sekondari mkoani Morogoro.
Ofisa Elimu wa Mkoa wa Morogoro, Fatma Kilimia, alitoa taarifa juzi
wakati wa kikao cha uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na kidato cha
kwanza mwakani.
Kilimia alisema kuwa kati ya waliokosa nafasi za kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza licha ya kufaulu mitihani yao.
“ Tujipange kuwezesha kujenga madarasa haya ,tusisahau pia suala la
vyoo na nyumba za walimu na ujenzi huu uwe umekamilika kabla ya Februari
mwakani, ili watoto wasichelewe katika masomo yao,” alisema Kilimia.
Alisema wanafunzi walioandikishwa Machi mwaka huu kwa ajili ya
kufanya mtihani walikuwa ni 51,775 kati ya hao wavulana 24,979 na
wasichana walikuwa ni 26,796.
Wanafunzi 869 kati yao wavulana 468 na wasichana 401 walishindwa
kufanya mitihani kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vifo, utoro na
mimba.
Kwa mujibu wa Ofisa Elimu wa Mkoa huo, wanafunzi waliochaguliwa ni 30,808. Wavulana ni 15,161 na wasichana 15,647.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Halima Dendego, aliwataka wakurugenzi
watendaji kwa kushirikiana na madiwani pamoja na wananchi kutumia muda
mfupi uliobakia kujenga vyumba vya madarasa vinavyohitajika ili
kuwezesha watoto wote waliofaulu kuingia darasani kabla ya muhula wa
mwaka wa masomo kuanza.
MALI YA TAIFA.. ISIYOKUWA NA FAIDA KWA MWANANCHI.
 |
| TWIGA |
UBOVU WA BARABARA MAENEO YA SINZA.
 |
| Maeneo ya sinza. |
Kiukwe naweza kusema hii imekuwa kero kubwa sana maeneo ya sinza kuanzia hapa kijueni kurudi nyuma kamaunarudi pande za magomeni kiukweli barabara ni mbovu !! mbovu!! mbovu!!! kupita kiasi. hii ni kasumba kubwa sana. na ukiuliza. kwanini barabara wakazi wa maeneo hayo. wanakwambia wamechoshwa na ahadi za viongozi wao. kitaswira na kimuonekano ni kwamba viongozi wetu pale wanapotaka kura zenu. utumia neno la kusema hivi. barabara juu na chini. ili tu wananchi waamini. lakini sasa imekuwa kero sana hasa kwa wakazi wa sinza. na ukiuliza je viongozi hao huwa wanapita maeneo hayo. wakazi hao watakujibu ndio. lakini hii inatokana na dharau za viongozi wetu kwa kuwadharau wananchi. viongozi hao wamekuwa wakipita na magari yao ya kifahari yaliyo tokana pesa za wananchi. nakumbuka kipindi cha kampeni kuna kiongozi alitamka neno hili. nitajenga barabra zote kwa kiwango cha lami. na pia barabara za juu. Lakini sasa imekuwa kwamba kama kiongozi atatoa ahadi za uongo. na asitekeleze je wananchi watamuamini tena? jibu ni hapana. kiukweli kama mtu au kiongozi hawezi kutekeleza jambo ni bora asema hivi, nitatoa huduma kwa kadiri nitakavyo weza. aliye yasema maneno hayo ni rais wetu. siwezi kuacha kumtaja maana nisipo mtaja nitakuwa mnafiki... Jamani viongozi inaonyesha hata familiya zenu mnazidanganya hivyo. kama uongo na ahadi kama hivi mtaendelea nazo. kiukweli mnapeleka taifa kubaya sana na si kingine ni kizai kijacho. HII NI CHANGA MOTO KWA VIONGOZI. NAWAOMBA HIZO PAMBA MLIZO WEKA MASIKIONI ZITOENI.