Michezo

Barclays Msimamo wa Ligi Kuu ya England

Jumanne, 24 Mei 2011 11:03 UK
Position Timu M TG PNT
Full Barclays Msimamo wa Ligi Kuu ya England
1 Man Utd 38 41 80
2 Chelsea 38 36 71
3 Man City 38 27 71
4 Arsenal 38 29 68
5 Tottenham 38 9 62
6 Liverpool 38 15 58
7 Everton 38 6 54
8 Fulham 38 6 49
9 Aston Villa 38 -11 48
10 Sunderland 38 -11 47
11 West Brom 38 -15 47
12 Newcastle 38 -1 46
13 Stoke 38 -2 46
14 Bolton 38 -4 46
15 Blackburn 38 -13 43
16 Wigan 38 -21 42
17 Wolves 38 -20 40
18 Birmingham 38 -21 39
19 Blackpool 38 -23 39
20 West Ham 38 -27 33

Ancelotti atimuliwa umeneja wa Chelsea


Chelsea imemtimua meneja wake Carlo Ancelotti baada ya kumaliza msimu wake wa pili bila kombe lolote.
Carlo Ancelotti
Carlo Ancelotti
Alitimuliwa baada ya Chelsea kumaliza Ligi msimu huu kwa kuchapwa bao 1-0 na Everton na klabu hiyo ikimaliza kwa kushika nafasi ya pili ya msimamo wa Ligi Kuu ya Soka ya England.
Ancelotti mwenye umri wa miaka 51 mkataba wake ulikuwa umalizike mwakani katika klabu ya Chelsea.
Taarifa ya klabu hiyo imesema: "Matumaini yetu kwa msimu huu yamekuwa mabaya kutokana na matokeo tuliyopata tofauti na tulivyotarajia na klabu inaona ni sawa kabisa kufanya mabadiliko haya kwa ajili ya maandalizi mazuri ya msimu ujao."
Wameshindwa kubeba kombe la Ubingwa wa Ligi na kuikodolea macho Manchester United ikichukua kombe hilo kwa mara ya 19 wiki moja iliyopita, pia Chelsea wakatolewa katika mbio za kuwania Ubingwa wa Vilabu kwa nchi za Ulaya, wakatupwa nje kombe la FA na vilevile kuwania Kombe la Carling msimu huu.
Chelsea ambao walikuwa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu na Kombe la FA msimu huu uliopita, wamemaliza pointi tisa nyuma ya Manchester United na wamewatangulia Manchester City walioshika nafasi ya tatu kwa tofauti ya mabao tu.
Meneja wa zamani wa klabu hiyo Avram Grant naye alikumbana na hali kama hiyo wakati Chelsea ilipomaliza nafasi ya pili katika Ligi Kuu ya England na ikashindwa katika fainali ya Ubingwa wa Ulaya mwaka 2008 kwa mikwaju ya penalti.
Na mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich, aliyemsajili Fernando Torres kwa kitita cha paundi milioni 50 wakati wa usajili mdogo mwezi wa Januari, sasa ataanza hekaheka za kumpata meneja mwengine mwenye uwezo wa kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu kutoka kwa Manchester United na pia tamaa kubwa ya klabu hiyo ya kubeba kombe la klabu bingwa ya Ulaya.

 


Mali: Mabadiliko ya kura Kombe la Dunia:


Rais wa Shirikisho la Soka la Mali Hammadoun Kolado Cisse ametaka mabadiliko yafanyike ya mfumo wa upigaji kura kutafuta nchi itakayoandaa Kombe la Dunia.
Kombe la Dunia la soka
Kombe la Dunia la soka
Pia amesema bado hajaamua nani atampigia kura katika uchaguzi unaokuja wa Rais wa Fifa.
Kauli hiyo ameitoa licha ya Shirikisho la Soka barani Afrika kueleza litamuunga mkono Rais wa sasa wa Fifa Sepp Blatter na sio mpinzani wake pekee Mohamed Bin Hammam.
"Kwa wakati huu siwezi kuzungumzia mgombea gani tutakayemuunga mkono," alisema Cisse.
Katika mkutano uliofanyika mjini Cairo siku ya Jumatatu, Shirikisho la Soka barani Afrika, lilisema kamati yake kuu imekuwa na kura ya siri na imepitisha muswda wa kumuunga mkono Blatter katika uchaguzi wa Fifa.
"Kamati kuu inaweza kutoa mapendekezo, lakini chama au shirikisho la soka la nchi huamua kivyake nani wa kumpigia kura," Cisse alifafanua.
"Hawapaswi kufuata mapendekezo ya kamati na baadhi ya nchi zinamuunga mkono Blatter na nyingine bin Hammam.
"Tunataka mabadiliko ya kweli ndani ya Fifa - namna tunavyofanya kazi, jinsi usimamizi wa fedha ulivyo - lakini siwezi kusema iwapo hicho ndio kigezo cha kubadilisha Rais."
Cisse anataka Mkutano Mkuu wa Fifa kuliko wajumbe 24 wa kamati ya utendaji kutoa uamuzi wa mwisho ni nchi gani ya kuandaa Kombe la Dunia.
Mchakato huo umezongwa na tuhuma za rushwa.
"Iwapo kila nchi itaweza kupiga kura kwa nchi itakayoandaa Kombe la Dunia, hiyo itasaidia sana kupunguza tuhuma za rushwa kwa sababu huwezi kuhonga vyama na mashirikisho 203 ya soka."
Cisse ameongeza kundi la nchi za Afrika litashauri mabadiliko haya kabla ya uchaguzi haujafanyika tarehe 1 mwezi wa Juni, lakini akakataa kusema iwapo nchi nyingine zitaunga mkono.
Pia amesema angefurahi mfumo wa wajumbe wa Kamati Kuu ya Fifa nao ungeangaliwa na kuwa na wajumbe zaidi ya wanne wa sasa kutoka nchi za Afrika.


                                                                                                                                                           

Ferguson aonywa na FA dhidi ya mwamuzi

Tume ya mienendo ya Chama cha England-FA, imemuonya Sir Alex Ferguson kuhusiana na matamshi yake siku zijazo baada ya matamsi yake dhdi ya mwamuzi Howard Webb.
Sir Alex Ferguson
Sir Alex Ferguson
Matamshi hayo yalitolewa na meneja huyo wa Manchester United kabla ya mchezo wao wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Chelsea, ambapo Manchester United ilishinda mabao 2-1 tarehe 8 mwezi wa Mei.
Licha ya Ferguson kumzungumzia Webb, amevunja taratibu za FA ambapo meneja yeyote hatakiwi kumzungumzia mwamuzi kabla ya mchezo.
"Alivunja taratibu kwa kiasi kidogo, lakini hata hivyo alikiuka taratibu," taarifa ya FA iliongeza.
Mwenyekiti wa tume hiyo alisema: "Taratibu za uamuzi huu ziliwekwa mwanzoni mwa msimu wa 2009/10 na ukarudiwa tena rasmi kwa vilabu tarehe 21 mwezi wa Oktoba 2010.
"Huku ni kwenda kinyume na taratibu zilizowekwa na ni mara ya kwanza hoja hiyo kusikilizwa na tume.
"Matokeo yake kuhusiana na mashtaka haya, tume ilikuwa ikifahamu juu ya matukio mengine ambapo matamshi kabla ya mechi yalitolewa na mameneja wengine.
"Katika shauri hili, ilichukuliwa kama ni kuvunjwa kwa taratibu kwa kiasi kidogo na onyo litolewe kwa mameneja wote kwa siku zijazo kwamba wakienda kinyume na taratibu, hata wakitoa matamshi ya mazuri ambayo pengine yataharibu amani, hatua kali zitachukuliwa dhidi yao."
Siku mbili kabla ya mchezo baina ya Manchester United dhidi ya Chelsea - ambapo Chelsea wangeshinda wangeongoza msimamo wa ligi - Ferguson katika mkutano na waandishi wa habari alimzungumzia Webb.
Wakati huo alisema: "Tumempata mwamuzi mzuri, hakuna shaka yoyote kuhusiana na hilo."
"Lakini wasiwasi wetu mkubwa ni kupata matokeo mabaya."
"Tunao wachezaji wazuri wa kufanya vizuri. Tunatumai ni wakati wetu kupata angalao bahati kidogo."
Ni hivi karibu Ferguson alimaliza adhabu yake ya kufungiwa kukaa katika benchi la ufundi la timu yake kwa michezo mitano na pia alipigwa faini ya paundi 30,000kutokana na kumshutumu mwamuzi Martin Atkinson baada ya kufungwa mabao 2-1 na Chelsea mwezi wa Machi.
                                                                                                                                                                     

West Ham kupata meneja mpya karibuni

West Ham ina matumaini itamteua meneja mpya katika muda wa wiki mbili au tatu zijazo baada ya kuachana na Avram Grant.
Avram Grant
Avram Grant
Klabu ya West Ham ilitangaza kumtimua Grant siku ya Jumapili baada ya kuchapwa mabao 3-2 dhidi ya Wigan, hali iliyosababisha wateremke daraja.
Kocha wa zamani wa timu ya taifa ya England Steve McClaren ni mmoja kati ya makocha wanaopewa nafasi kubwa ya kurithi kazi ya Grant.
Kocha wa kikosi cha kwanza Kevin Keen ndiye atakamata hatamu kwa muda na yeye pamoja na meneja wa zamani wa Newcastle Chris Hughton wanapewa nafasi baada ya McClaren.
Wengine wanaotajwa huenda wakachukua nafasi ya umeneja wa West Ham ni pamoja na Neil Warnock meneja wa sasa QPR, meneja wa zamani wa Bolton, Newcastle na Blackburn Sam Allardyce na mlinzi wa zamani wa West Ham Slaven Bilic.
Grant alichukua nafasi ya Jose Mourinho kuwa meneja wa Chelsea mwezi wa Septemba mwaka 2007, na akatimuliwa baada ya kuifikisha timu hiyo katika fainali ya Ubingwa wa vilabu vya Ulaya, ambapo walifungwa kwa mikwaju ya penalti na Manchester United.
Mwezi wa Novemba mwaka 2009 alichukua nafasi ya kuifundisha Portsmouth, lakini pamoja na mzozo wa kifedha, hakuweza kuisaidia klabu hiyo kushuka daraja.
Wamiliki wa West Ham David Gold na David Sullivan walimchukua Grant mwenye umri wa miaka 56, wakiwa na matumaini angeweza kuijenga West Ham imara katika Ligi Kuu ya Soka ya England.
Waliweza kuwasajili nahodha wa timu ya taifa ya Ujerumani Thomas Hitzlsperger, Frederic Piquionne na Pablo Barrera.
Hali ya kukata tamaa nusu ya kwanza ya msimu, iliibua taarifa huenda Grant nafasi yake ingechukuliwa na Martin O'Neill, lakini Grant aliendelea na kazi yake na akaruhusiwa kuwachukua wachezaji wengine akiwemo Demba Ba, Robbie Keane, Wayne Bridge na Victor Obinna.
Na bahati ya klabu hiyo ilionekana kunawiri pale waliposhinda mechi tatu kati ya tano mwezi wa Februari na Machi, ikiwemo ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Liverpool.
Lakini kufungwa na Wigan ilikuwa ni mara ya sita kwao katika michezo saba ya ligi, na kuwaacha wakiwa pointi sita nyuma chini kabisa ya jedwali na uongozi wa klabu ukaonelea wakati sasa umefika wa kufanya mabadiliko
                                                                                                                                                                  

Barclays Msimamo wa Ligi Kuu ya England


Asabar, 21 Mei 2011 00:00 UK
Position Timu M TG PNT
Full Barclays Msimamo wa Ligi Kuu ya England
1 Man Utd 37 39 77
2 Chelsea 37 37 71
3 Man City 37 25 68
4 Arsenal 37 29 67
5 Tottenham 37 8 59
6 Liverpool 37 16 58
7 Everton 37 5 51
8 Fulham 37 6 48
9 Stoke 37 -1 46
10 Bolton 37 -2 46
11 West Brom 37 -15 46
12 Newcastle 37 -1 45
13 Aston Villa 37 -12 45
14 Sunderland 37 -14 44
15 Blackburn 37 -14 40
16 Wolves 37 -19 40
17 Birmingham 37 -20 39
18 Blackpool 37 -21 39
19 Wigan 37 -22 39
20 West Ham